Mshindi wa mbio za umbali wa Km 42 Kipkemoi Kipsang wa Kenya akimalizia mbio hizo kwenye Uwanja wa Chuo cha Ushirika Moshi katika mashindano ya Kimataifa ya Kilimanjaro 2011.Alizawadiwa sh. miloni 3.
Mshindi wa kwanza wa mbio za umbali wa Km 42 kwa upande wa wanawake, Anna Kamau kutoka Kenya akimalizia mbio hizo kwenye Uwanja wa Chuo cha Ushirika Moshi katika mashindano ya Kimataifa ya Kilimanjaro 2011.Alizawad iwa sh. miloni 3.
Mshindi wa kwanza wa mbio za Km 42,Kipkemoi Kipsang (kulia) wa Kenya akichuana vikali na mkenya mwenzie Julius Kilimo muda mfupi kabla ya kumaliza mbio hizo. Kilimo alishinda nafasi ya pili.
Newar Twist akikimbia na mbwa wake,Barney Twist katika mashindano ya mbio za Km 21 katika mashindano ya kimataifa ya Kilimanjaro 2011, mjini Moshi leo.Yeye na mbwa wake walimaliza mbio ambapo hata mbwa alikabidhiwa medali na fulana vitu ambavyo kila mshiriki wa mashindano hayo alipatiwa.
Mmoja wa washiriki wa mashindano hayo akikimbia huku akiwa na bendera ya Taifa jana eneo la Mwika.(PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)



































